102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

 102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

 

1.   

Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka;

Na kuvaa kutokuharibika,

Nitamjua Mwokozi nifikapo ng’amboni;

Atakuwa wa kwanza kunilaki.

 

Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;

Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.

 

2.   

Furaha nitapata nikiona makao

Bwana aliyotuandalia;

Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo

Vilivyonipa pahali Mbinguni.

 

3.   

Nao waliokufa katika Bwana Yesu,

Nitawaona tena huko juu;

Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni,

Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

 

4.   

Milangoni mwa mji Bwana atanipisha,

Pasipo machozi wala huzuni.

Nitauimba wimbo wa milele; lakini

Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)