104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say) 

 

1.   

Twasoma, ni njema sana

Mbinguni, kwa Bwana;

Twasoma, dhambi hapana,

Mbinguni kwa Bwana;

Malaika wema wako,

Vinanda vizuri viko,

Na majumba tele yako,

Mbinguni kwa Bwana.

 

2.   

Siku zote ni mchana,

Ni nchi ya raha;

Wala machozi hapana,

Ni nchi ya raha;

Walioko wauona

Uso wa Mwokozi, tena

Jua jingine hapana,

Ni nchi ya raha.

 

3.   

Nyama na vitu viovu

Havimo kabisa;

Kifo nacho, na ubovu,

Havimo kabisa.

Ni watakatifu wote,

Wameoshwa dhambi zote;

Wasiosafiwa wote

Hawamo kabisa.

 

4.   

Tuna dhambi, pia sote,

Mwokozi akafa;

Kwake tutaoshwa zote,

Mwokozi akafa;

Kwake twapata wokovu,

Tutawona utukufu;

Mbinguni tutamsifu;

Mwokozi akafa.

 

5.   

Baba, mama, ndugu zetu,

Twendeni kwa Bwana;

Huku chini sio kwetu,

Twendeni kwa Bwana;

Tusishikwe na dunia,

Na dhambi kutulemea;

Tutupe vya chini pia,

Twendeni kwa Bwana.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)