103. Kaa Nami (Abide with me)

103. Kaa Nami (Abide with me)

 

1.   

Kaa nami, ni usiku tena;

Usiniache gizani, Bwana;

Msaada wako haukomi;

Nili peke yangu, kaa nami.

 

2.   

Siku zetu hazikawi kwisha,

Sioni la kunifurahisha;

Hakuna ambacho hakikomi,

Usiye na mwisho kaa nami.

 

3.   

Nina haja nawe kila saa;

Sina mwingine wa kunifaa;

Mimi nitaongozwa na nani

Ila wewe Bwana, kaa nami.

 

4.   

Sichi neno uwapo karibu;

Nipatalo lote, si taabu;

Kifo na kaburi haviumi;

Nitashinda kwako, kaa nami.

 

5.   

Nilalapo nikuone wewe,

Gizani mote nimulikie;

Nuru za mbinguni hazikomi,

Siku zangu zote kaa nami.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)