108. Twenende Sayuni (We're marching to Zion)

 108. Twenende Sayuni (We're marching to Zion)

 

1.   

Mpendao Bwana

Ije raha yenu!

Imbeni nyimbo za raha

Wa ibada yenu.

 

Twenende Sayuni,

Mji mzuri Sayuni;

Twenende juu Sayuni

Ni maskani ya Mungu.

 

2.   

Wasiimbe wao

Wasioamini,

Watoto wa Mungu ndio

Waimbao chini.

 

3.   

Twaona rohoni

Baraka za Mungu,

Tusijafika Mbinguni

Kwenye utukufu.

 

4.   

Tutakapo mwona

Masumbuko basi,

Huwa maji ya uzima,

Anasa halisi.

 

5.   

Tupaaze sauti,

Na fute machozi,

Twenenda kwa Imanweli

Naye ni Mwokozi.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)