111. Neno Lako Bwana (Lord, thy word abideth)

 111. Neno Lako Bwana (Lord, thy word abideth)

 

1.   

Neno lako, Bwana,

Ni imara sana;

Lilo latwongoza,

Lilo latufunza.

 

2.   

Adui wabaya

Wakikaribia,

Neno lake Bwana

Ni ulinzi sana.

 

3.   

Siku za dhoruba

Soma ukiomba;

Neno lake Bwana

Msaada sana.

 

4.   

Ukiliamini,

Hwenda na amani;

Una na furaha

Neno ni silaha.

 

5.   

Ni furaha kweli,

Na wingi wa mali,

Neno lake Bwana

Kwa wasiokana.

 

6.   

Neno la rehema,

Tukali wazima;

Faraja i papo,

Tufarikanapo.

 

7.   

Tulijue sana,

Neno lako, Bwana,

Hapa tukupende,

Kisha kwako twende.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)