111. Neno Lako Bwana (Lord, thy word abideth)
111. Neno Lako Bwana (Lord, thy word abideth)
1.
Neno lako, Bwana,
Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.
2.
Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.
3.
Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.
4.
Ukiliamini,
Hwenda na amani;
Una na furaha
Neno ni silaha.
5.
Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana.
6.
Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja i papo,
Tufarikanapo.
7.
Tulijue sana,
Neno lako, Bwana,
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.
Comments
Post a Comment