113. Ni Mfalme wa Mapenzi (The King of love my Shepherd is)

113. Ni Mfalme wa Mapenzi (The King of love my Shepherd is)

 

1.   

Ni Mfalme wa mapenzi

Ndiye anichungaye,

Sipungukiwi, hawezi.

Kunipoteza yeye.

 

2.   

Kando ya maji mazima

Yeye huniongoza

Katika malisho mema

Daima hunilaza.

 

3.   

Mara nyingi hupotea

Kwa ukaidi wangu,

Naye huniandamia,

Hunirudisha kwangu.

 

4.   

Uvulini mwa mauti,

Sichi hatari kamwe,

Wewe Bwana huniachi,

Mwokozi wangu Wewe.

 

5.   

Waniandikia meza

Neema kwako tele.

Kwa Wewe, yote naweza.

Na msalaba mbele.

 

6.   

Kamwe hautapungua

Uule wema wako;

Mwisho, atanichukua,

Juu, niimbe kwako.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)