114. Bwana Mungu, Nashangaa Kabisa (How great thou art)

114. Bwana Mungu, Nashangaa Kabisa (How great thou art)

 

1.   

Bwana Mungu, nashangaa kabisa

Nikitazama kama vilivyo

Nyota, ngurumo, vitu vingi vyote

Viumbwavyo kwa uwezo wako.

 

Roho yangu na ikuimbie

Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,

Roho yangu na ikuimbie

Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.

 

2.   

Nikitembea pote duniani,

Ndege huimba, nawasikia,

Milima hupendeza macho sana,

Upepo nao nafurahia.

 

3.   

Nikikumbuka kama Wewe Mungu

Ulivyompeleka Mwanao,

Afe azichukue dhambi zetu,

Kuyatambua ni vigumu mno.

 

4.   

Yesu Mwokozi utakaporudi

Kunichukua kwenda Mbinguni,

Nitashukuru na kwimba milele,

Wote wajue jinsi ulivyo.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)