120. Enyi Wanadamu (Souls of men, why will ye scatter?)

120. Enyi Wanadamu (Souls of men, why will ye scatter?)

 

1.   

Enyi wanadamu mbona

Sana mwatanga-tanga,

Kama kondoo wanyonge,

Wasio na mchunga?

Yuko mchunga mmoja

Mwenye mapenzi mema;

Haya kutaneni kwake,

Atawachunga vyema.

 

2.   

Mungu tunamwona kuwa

Mwenye uwezo wote;

Na nguvu zake zapita

Mawazo yetu yote:

Ni Baba,mapenzi yake

Ni makubwa hakika;

Hatuwezi kuyajua,

Na hayana mpaka.

 

3.   

Rehema za Mungu nazo

Zina upana sana;

Kama huo wa bahari,

Mwisho wake hapana;

Haki yake ina mema,

Kwa hayo twashukuru,

Kwetu uko msamaha,

Furaha na uhuru.

 

4.   

Mapenzi yake mapana,

Sisi hatuna cheo

Cha kutosha, nao moyo

Una wema upeo;

Ukombozi mwingi mno

Katika damu yake;

Sote twapata furaha,

Kwa maumivu yake.

 

5.   

Yesu mkaribieni

Njoni msife myoyo;

Njoni kwake kwa imani,

Mema yake ni hayo;

Heri tuwe kama wana

Tushike neno lake,

Daima atatujaza

Tele furaha yake.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)