122. Bwana Yesu

122. Bwana Yesu

 

1.   

Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unaumia? Unateseka sana,

Kwa ajili ya kuomba,

Waomba na jasho jingi likageuka damu.

 

Kumbe! Ni dhambi zangu zinazokuumiza.

Bwana wangu, Mungu wangu,

Mimi leo, naja kwako

Ili niziungame.

 

2.   

Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unaumia, na mizigo mizito?

Umejitwalia wewe, msalaba mabegani

Kwa ajili ya watu.

 

3.  

Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unatukanwa, wawambwa kama mwizi,

Bila kosa ukalia, Baba yangu, wasamehe,

Chukua roho yangu.

 

4.   

Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Muda ulipofika, nchi ikawa giza,

Mbinguni pakatulia,

Angani pakawa kimya,

Watu wakaogopa.

 

5.   

Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Jinsi ulivyoumwa, ukamwomba Baba,

Leo umeshinda kifo, sasa wapaa Mbinguni,

Naimba, Haleluya.

Comments

Popular posts from this blog

101. Twonane Milele (In the sweet by-and-by)

102. Kazi Yangu Ikiisha (When my life work is ended)

104. Twasoma ni Njema Sana (There is a better world they say)